SEHEMU YA PILI
WATUNZI- wastara juma na @hadithizetu
Whatsapp 0769510060.
Nililia sana baada ya kuwapoteza wazazi wangu wote, nilihisi
hata maumivu ya kuingiliwa kinguvu na wanaume nane yameisha kabisa, kilicho
niuma nipale mme wangu alipo pata taarifa ya kuja kuwaaga wazazi wangu kwenye
msiba lakini alikataa kabisa kuja sababu mke wake alimzuia, Baada ya mazishi
kuisha, niliendelea kukaa na mdogo wangu ambae alikuwa anaishi palepale
nyumbani na wazazi, lakini baada ya wiki chache nikaanza kujisikia utofauti
mwilini mwangu, kumbe nilikuwa nimepata ujauzito kutoka kwa wale vijana walio
nibaka! ujauzito ulinishangaza maana nilijihisi wa furaha vilevile nikajiona wa
uzuni pia maana mme wangu alikuwa anasema sina uwezo wa kuwa na mtoto ila chakushangaza
nilivyo bakwa nikapata ujauzito.
Maisha yaliendelea taratibu huku tumbo likiendelea kukuwa,
baada ya miezi sita Janeth ambae ni mdogo wangu wa kike akawa amepata mchumba,
na hawakukaa hata siku nyingi akawa amechukuliwa nyumbani hivyo nikaanza kuishi
mwenyewe pale nyumbani. Nilicho mshukuru Mungu mdogo wangu alikuwa anakuja
kunitembelea hivyo sikujihisi mpweke sana, na hata mme wake pia alimruhusu
kwamba awe anakuja kunitembelea maana nilikuwa nachoka sana kutokana na ule
ujauzito, kuna kipindi ambacho siwezi kusahau kabisa maana ilikuwa imebaki
mwezi mmoja tu nijifungue lakini kwa bahati mbaya mme wake Janeth akaugua sana,
ikabidi mdogo wangu akamuangalie mme wake kwanza maana alikuwa na hali mbaya
kiafya.
Ujauzito ulinitesa sana, maana sikuwa na mtu wa kunisaidia,
kibaya zaidi hata ndugu zetu baada ya msiba hakuna hata mmoja alieweza kuja
kututembelea pale nyumbani, tumbo lilikuwa linanisumbua sana na sikuwa na pesa
ndani hivyo ilinibidi niwe napalilia mwenyewe shambani ili niweze kupata chakula,
hata nilipo umwa sana nilikuwa natumia dawa za kyenyeji maana hospitalini palikuwa
mbali na hata hivyo pesa ya matibabu sikuwa nayo kabisa.
Maisha yaliendelea kuwa magumu sana mpaka nikaipoteza furaha
nikawa mtu wa mawazo sana, sikuwa na mtu wa kumdekea maana kipindi mama yupo
hai mda mwingine alikuwa anatufariji wanae.
Siku moja usiku mvua ikiwa inanyesha sana, nilipata uchungu
wa kujifungua, sikuwa na mtu yoyote pale nyumbani wa kunisaidia na nilikuwa
nasikia mtoto anatoka, nilianza kupiga kelele maana ilikuwa mida kama ya saa
nane lakini hakuna hata mmoja alie sikia nje, hali ilikuwa ngumu nguvu
zikaniishia kabisa nikajua moja kwa moja lazima nife na mtoto afe tu, kipindi
natapatapa huku na kule mule ndani, huku mvua kubwa inanyesha, kumbe kuna mkaka
mmoja alikuwa anapita usiku uleule na baiskeli akaona bora ajikinge pale
nyumbani, sasa wakati yupo kwa nje akasikia mimi nalia kwa ndani, ndipo akaanza
kugonga mlango ili nimfungulie, nilipo sikia mtu anagonga nikatamani kuamka ili
nimfungulie anisaidie, lakini nilipo jaribu kuamka tu nilianguka hapohapo nguvu
sina ila nikasema nikizubaa tu namuua mwanangu ndipo nikaanza kujivuta kama
nyoka ili niufikie mlango kusudi niweze kusaidiwa ili mtoto atoke salama.
USIKOSE SEHEMU
YA TATU
WATUNZI wastara
juma na @hadithizetu
Kwa hadithi
nyingi zaidi follow @hadithizetu
Whatsapp group
0769510060
Post a Comment